-----------------------------------
BINAFSI
-----------------------------------
OGOPA watu wakimya. Ni rahisi watu kama hawa kufurahi kama ilivyo katika kukasirika. Na wanapofurahi hudhihirisha hili. Wanapokasirika hulizuia kwa ndani. Na wao kupasuka kama bomu ni kitu cha kawaida. Kama una mtu wa nanmna hii yapaswa uwe karibu naye sana.
------------------------------
NYUMBANI-------------------------------
NYUMBA kwa wengi wetu sio zaidi ya chumba cha kulala na choo. Ni nadra sana kwa baadhi yetu kuona hali katika maeneo mengine ya nyumba. Jenga tabia ya kukimbia chumba na choo chako ili uone wanao chini ya paa lako wanaishi vipi.
--------------------------------
NJIANI---------------------------------
NJIANI sio mahala pa makelele labda katika hali isiyo ya kawaida. Watu na jamii iliyostaarabika huonekana sio katika majumba yao tu bali pia wanavyochanganyika na watu wengine. Mtu mstaarabu kwa ndani anaweza akawa mshenzi wa mwisho barabarani.
--------------------------------
SAFARINI--------------------------------
KUNA vitu kadhaa ambavyo ni muhimu kuwa navyo unapokuwa safarini. Kwa mfano, sindano ya kushonea nguo na vifungo, Vingine ni chana, brashi ya viatu na nguo. Aidha mswaki, dawa ya mswaki, sabuni na marashi. Muhimu zaidi hata hivyo ni dawa zinazokusaidia mara kwa mara, kama zile za malaria, kichwa na kuzuia kuharisha na kutapika.
---------------------------------
SHULENI-----------------------------------
FANI ya uigizaji na maigizo katika shule nyingi za msingi imekufa. Katika miaka hii ambayo nchi sasa ina televisheni na inatengeneza sinema ni muhimu kuirudisha fani hiyo kwa nguvu mpya. Hili sio lazima lingojee serikali. Shule na idara za serikali, sekta ya umma na sekta binafsi zinaweza kulifufua kwa faida ya kurahisisha kazi na biashara za wote.
---------------------------------
KAZINI-----------------------------------
KAZI inayokuweka mahala pamoja tu haiwezi kukupatia mshahara na maslahi mazuri. Ukitaka ufaidi kazi lazima uwe na kazi yenye safari mzomzo. Kwazo hizo utaweza kuweka mshahara wakao kama akiba na kuufanyia zaidi kazi za maendeleo badala ya kuwa ni tonge la mkono kwenda kinywani tu.
----------------------------------
NCHI ZA NJE----------------------------------
ITAKUWA ni kupunguza kwa kiasi kikubwa kwa balozi za Tanzania nchi za nje kujenga au kununua hosteli na kuzipendezesha zifanane fanane na hoteli za kitalii. Hosteli hizo zikiwepo Watanzania waendao nchi hizo watakuwa na mahala nafuu na salama zaidi kulala. Na siyo tu hayo bali watakuwa wanapata huduma muhimu pamoja na ushauri wa shule, biashara na uwekezaji palepale ubalozini.
-----------------------------------
BURUDANI----------------------------------
MICHEZO ya kuigiza ni burudani moja ya aina yake. Wakiwepo watunzi wa hadithi na waigizaji wazuri mchezo wa kuigiza unaweza kuwa ni starehe na wakati huo huo darasa juu ya jambo muhimu katika maisha au katika suala la uchumi, siasa na utamaduni wa jamii husika. Tufufueni michezo ya kuigiza kwa kwenda mbele.
----------------------------------
MICHEZONI----------------------------------
MICHEZO bila washangiliaji sio mchezo. Na watu wachache kwa tamaa zao wanaweza kupandisha viingilio kiasi visilingane na thamani ya fedha apatayo mteja lakini hili siku moja litawatumbukia nyongo.
Lazima pawepo na njia za kisayansi za kukadiria nini iwe kiingilio cha kuingia katika shughuli fulani. Vinginevyo ni wizi!
-----------------------------------
MJINI-------------------------------------
MJINI ni mahala pa biashara. Na wafanyabiashara wengi ni wapangaji wa nyumba za watu wengine. Na inajulikana jinsi mpangaji au wapangaji fulani wanavyoweza kuzozana na mwenye nyumba. Wakifukuzwa wakaja wengine, je, ipo haki kwa shirika kama TANESCO kuwanyima umeme wapangaji wapya au TANESCO haijui biashara na inaendelea kuomba ruzuku tu toka serikalini ?
-------------------------------------
VIJIJINI-------------------------------------
KUNA vijiji ambavyo havistahili kuwa na tatizo la kukosa chakula kwa kuwa kuna mifereji ya maji ya kunyweshea mashamba. Kazi ni kutunza na kuendeleza mifumo hiyo ya umwagiliaji kwa namna isiyo na ujanja au upendeleo. Vijiji kama hivyo sio tu vitajitosheleza kwa mahitaji yao ya chakula bali pia vitauza ziada kwenye vijiji na miji mingine.
sammy.africa2100@gmail.com
Tuesday, December 1, 2009
ishi -- Alhamisi Desemba 3. 2990
-----------------------------------
BINAFSI-----------------------------------
OGOPA watu wakimya. Ni rahisi watu kama hawa kufurahi kama ilivyo katika kukasirika. Na wanapofurahi hudhihirisha hili. Wanapokasirika hulizuia kwa ndani. Na wao kupasuka kama bomu ni kitu cha kawaida. Kama una mtu wa nanmna hii yapaswa uwe karibu naye sana.
------------------------------
NYUMBANI-------------------------------
NYUMBA kwa wengi wetu sio zaidi ya chumba cha kulala na choo. Ni nadra sana kwa baadhi yetu kuona hali katika maeneo mengine ya nyumba. Jenga tabia ya kukimbia chumba na choo chako ili uone wanao chini ya paa lako wanaishi vipi.
--------------------------------
NJIANI---------------------------------
NJIANI sio mahala pa makelele labda katika hali isiyo ya kawaida. Watu na jamii iliyostaarabika huonekana sio katika majumba yao tu bali pia wanavyochanganyika na watu wengine. Mtu mstaarabu kwa ndani anaweza akawa mshenzi wa mwisho barabarani.
--------------------------------
SAFARINI--------------------------------
KUNA vitu kadhaa ambavyo ni muhimu kuwa navyo unapokuwa safarini. Kwa mfano, sindano ya kushonea nguo na vifungo, Vingine ni chana, brashi ya viatu na nguo. Aidha mswaki, dawa ya mswaki, sabuni na marashi. Muhimu zaidi hata hivyo ni dawa zinazokusaidia mara kwa mara, kama zile za malaria, kichwa na kuzuia kuharisha na kutapika.
---------------------------------
SHULENI-----------------------------------
FANI ya uigizaji na maigizo katika shule nyingi za msingi imekufa. Katika miaka hii ambayo nchi sasa ina televisheni na inatengeneza sinema ni muhimu kuirudisha fani hiyo kwa nguvu mpya. Hili sio lazima lingojee serikali. Shule na idara za serikali, sekta ya umma na sekta binafsi zinaweza kulifufua kwa faida ya kurahisisha kazi na biashara za wote.
---------------------------------
KAZINI-----------------------------------
KAZI inayokuweka mahala pamoja tu haiwezi kukupatia mshahara na maslahi mazuri. Ukitaka ufaidi kazi lazima uwe na kazi yenye safari mzomzo. Kwazo hizo utaweza kuweka mshahara wakao kama akiba na kuufanyia zaidi kazi za maendeleo badala ya kuwa ni tonge la mkono kwenda kinywani tu.
----------------------------------
NCHI ZA NJE----------------------------------
ITAKUWA ni kupunguza kwa kiasi kikubwa kwa balozi za Tanzania nchi za nje kujenga au kununua hosteli na kuzipendezesha zifanane fanane na hoteli za kitalii. Hosteli hizo zikiwepo Watanzania waendao nchi hizo watakuwa na mahala nafuu na salama zaidi kulala. Na siyo tu hayo bali watakuwa wanapata huduma muhimu pamoja na ushauri wa shule, biashara na uwekezaji palepale ubalozini.
-----------------------------------
BURUDANI----------------------------------
MICHEZO ya kuigiza ni burudani moja ya aina yake. Wakiwepo watunzi wa hadithi na waigizaji wazuri mchezo wa kuigiza unaweza kuwa ni starehe na wakati huo huo darasa juu ya jambo muhimu katika maisha au katika suala la uchumi, siasa na utamaduni wa jamii husika. Tufufueni michezo ya kuigiza kwa kwenda mbele.
----------------------------------
MICHEZONI----------------------------------
MICHEZO bila washangiliaji sio mchezo. Na watu wachache kwa tamaa zao wanaweza kupandisha viingilio kiasi visilingane na thamani ya fedha apatayo mteja lakini hili siku moja litawatumbukia nyongo.
Lazima pawepo na njia za kisayansi za kukadiria nini iwe kiingilio cha kuingia katika shughuli fulani. Vinginevyo ni wizi!
-----------------------------------
MJINI-------------------------------------
MJINI ni mahala pa biashara. Na wafanyabiashara wengi ni wapangaji wa nyumba za watu wengine. Na inajulikana jinsi mpangaji au wapangaji fulani wanavyoweza kuzozana na mwenye nyumba. Wakifukuzwa wakaja wengine, je, ipo haki kwa shirika kama TANESCO kuwanyima umeme wapangaji wapya au TANESCO haijui biashara na inaendelea kuomba ruzuku tu toka serikalini ?
-------------------------------------
VIJIJINI-------------------------------------
KUNA vijiji ambavyo havistahili kuwa na tatizo la kukosa chakula kwa kuwa kuna mifereji ya maji ya kunyweshea mashamba. Kazi ni kutunza na kuendeleza mifumo hiyo ya umwagiliaji kwa namna isiyo na ujanja au upendeleo. Vijiji kama hivyo sio tu vitajitosheleza kwa mahitaji yao ya chakula bali pia vitauza ziada kwenye vijiji na miji mingine.
sammy.africa2100@gmail.com
BINAFSI-----------------------------------
OGOPA watu wakimya. Ni rahisi watu kama hawa kufurahi kama ilivyo katika kukasirika. Na wanapofurahi hudhihirisha hili. Wanapokasirika hulizuia kwa ndani. Na wao kupasuka kama bomu ni kitu cha kawaida. Kama una mtu wa nanmna hii yapaswa uwe karibu naye sana.
------------------------------
NYUMBANI-------------------------------
NYUMBA kwa wengi wetu sio zaidi ya chumba cha kulala na choo. Ni nadra sana kwa baadhi yetu kuona hali katika maeneo mengine ya nyumba. Jenga tabia ya kukimbia chumba na choo chako ili uone wanao chini ya paa lako wanaishi vipi.
--------------------------------
NJIANI---------------------------------
NJIANI sio mahala pa makelele labda katika hali isiyo ya kawaida. Watu na jamii iliyostaarabika huonekana sio katika majumba yao tu bali pia wanavyochanganyika na watu wengine. Mtu mstaarabu kwa ndani anaweza akawa mshenzi wa mwisho barabarani.
--------------------------------
SAFARINI--------------------------------
KUNA vitu kadhaa ambavyo ni muhimu kuwa navyo unapokuwa safarini. Kwa mfano, sindano ya kushonea nguo na vifungo, Vingine ni chana, brashi ya viatu na nguo. Aidha mswaki, dawa ya mswaki, sabuni na marashi. Muhimu zaidi hata hivyo ni dawa zinazokusaidia mara kwa mara, kama zile za malaria, kichwa na kuzuia kuharisha na kutapika.
---------------------------------
SHULENI-----------------------------------
FANI ya uigizaji na maigizo katika shule nyingi za msingi imekufa. Katika miaka hii ambayo nchi sasa ina televisheni na inatengeneza sinema ni muhimu kuirudisha fani hiyo kwa nguvu mpya. Hili sio lazima lingojee serikali. Shule na idara za serikali, sekta ya umma na sekta binafsi zinaweza kulifufua kwa faida ya kurahisisha kazi na biashara za wote.
---------------------------------
KAZINI-----------------------------------
KAZI inayokuweka mahala pamoja tu haiwezi kukupatia mshahara na maslahi mazuri. Ukitaka ufaidi kazi lazima uwe na kazi yenye safari mzomzo. Kwazo hizo utaweza kuweka mshahara wakao kama akiba na kuufanyia zaidi kazi za maendeleo badala ya kuwa ni tonge la mkono kwenda kinywani tu.
----------------------------------
NCHI ZA NJE----------------------------------
ITAKUWA ni kupunguza kwa kiasi kikubwa kwa balozi za Tanzania nchi za nje kujenga au kununua hosteli na kuzipendezesha zifanane fanane na hoteli za kitalii. Hosteli hizo zikiwepo Watanzania waendao nchi hizo watakuwa na mahala nafuu na salama zaidi kulala. Na siyo tu hayo bali watakuwa wanapata huduma muhimu pamoja na ushauri wa shule, biashara na uwekezaji palepale ubalozini.
-----------------------------------
BURUDANI----------------------------------
MICHEZO ya kuigiza ni burudani moja ya aina yake. Wakiwepo watunzi wa hadithi na waigizaji wazuri mchezo wa kuigiza unaweza kuwa ni starehe na wakati huo huo darasa juu ya jambo muhimu katika maisha au katika suala la uchumi, siasa na utamaduni wa jamii husika. Tufufueni michezo ya kuigiza kwa kwenda mbele.
----------------------------------
MICHEZONI----------------------------------
MICHEZO bila washangiliaji sio mchezo. Na watu wachache kwa tamaa zao wanaweza kupandisha viingilio kiasi visilingane na thamani ya fedha apatayo mteja lakini hili siku moja litawatumbukia nyongo.
Lazima pawepo na njia za kisayansi za kukadiria nini iwe kiingilio cha kuingia katika shughuli fulani. Vinginevyo ni wizi!
-----------------------------------
MJINI-------------------------------------
MJINI ni mahala pa biashara. Na wafanyabiashara wengi ni wapangaji wa nyumba za watu wengine. Na inajulikana jinsi mpangaji au wapangaji fulani wanavyoweza kuzozana na mwenye nyumba. Wakifukuzwa wakaja wengine, je, ipo haki kwa shirika kama TANESCO kuwanyima umeme wapangaji wapya au TANESCO haijui biashara na inaendelea kuomba ruzuku tu toka serikalini ?
-------------------------------------
VIJIJINI-------------------------------------
KUNA vijiji ambavyo havistahili kuwa na tatizo la kukosa chakula kwa kuwa kuna mifereji ya maji ya kunyweshea mashamba. Kazi ni kutunza na kuendeleza mifumo hiyo ya umwagiliaji kwa namna isiyo na ujanja au upendeleo. Vijiji kama hivyo sio tu vitajitosheleza kwa mahitaji yao ya chakula bali pia vitauza ziada kwenye vijiji na miji mingine.
sammy.africa2100@gmail.com
Monday, November 30, 2009
ishi - Desemba 2, 2009
BINAFSI
WATU wengi hudhani kulipiza kisasi au kumtendea ubaya aliyekutendea ubaya ndio jambo linalofaa. Jaribu kutolipiza kisasi na umtendee wema aliyekutendea ubaya. Lazima lipo litakalokushangaza tu.
NYUMBANI
ISRAFU ni matumizi mabaya kwa kile mnachoruzukiwa na aliyewaumba. Wafundishe jamaa yako 'uchumi' katika matumizi. Ziada inayozidi inaweza ikatolewa kwa wahitaji kwa baraka zaidi kwa familia yenu. Israfu ikiendelea bila kudhibitiwa hujenga familia isiyojali na isiyo na huruma.
NJIANI
KUWA mwangalifu na waendesha baiskeli na vijana wenye magurudumu miguuni. Tahadhari inahitajika sio tu kujihami mwenyewe bali pia kukuepusha wewe kuwa chanzo cha umauti au ulemavu kwa hao wapanda baiskeli na waburuza 'rolasketi' .
SAFARINI
SAFARINI huweza kugeuzwa sadaka au ibada ya aina fulani. Ukisafiri jenga mazoea ya kuulizia ndugu, jamaa au Watanzania wenzako wanapoishi. Kwalo hilo unaweza kupeleka faraja kwa wenye dhiki au maradhi. Na kama sehemu unaijua ni vizuri pia kutembelea hospitali za karibu. Afya yako ya mwili na akili yaweza kuimarika kwa hili.
KAZINI
MAHALA pa kazi huweza kugeuzwa kituo kizuri cha upatu au SACCOS jinsi mnavyotaka wenyewe. Ili mradi tu kuchagua watu waaminifu kusimamia shughuli yenyewe. Kuchanga shilingi elfu moja au mbili kwa wiki kunaweza kuja kukusaidia katika shida usiyotegemea.
SHULENI
KUSOMA sana sio kufaulu sana. Watazame wanaobukua usiku na mchana ulinganishe na matokeo yao bila shaka utawasikitikia. Kusoma kunahitaji kuweka mikakati na kutumia akili zaidi ya darasani.
NCHI ZA NJE
KAZI nyingine za nje ni kuwa boi au yaya nyumbani kwa mtu. Tofauti na hapa Tanzania ni ule ukweli kuwa mshahara ni mzuri na unaweza ukatuma fedha nyumbani. Ili mradi upate mwajiri anayemwogopa Mungu. Vinginevyo unaweza kunyanyasika huko kiasi cha kutisha. Chunguza kwanza kabla ya kuamua.
BURUDANI
Mchezo wa kurusha vishale (darts) ni burudani kwa watu wanaopenda starehe ya mchezo wa kikundi. Katika burudani hii unaweza kuzungumza na marafiki na jamaa; unaweza kunywa na mnaweza mkapanga mambo mbali mbali ya kufanya siku zijazo. Ni burudani inayochochea uvumbuzi, uzuzi na ujasiriamali.
MICHEZONI
WANAOHARIBU michezo wakati mwingine ni waandishi wa habari na vyombo vyao. Hivi sasa baadhi yao wanafundisha kuliko kocha, wanacheza kuliko mchezaji bora; na ni waamuzi wa kutegemea kuliko waamuzi wa mechi husika. Hili halisaidii michezo. Linabomoa michezo.
MJINI
KATIKA miji yetu mingi hivi sasa jenga mazoea ya kutazama mguu wako unakotua. Katika baadhi ya mitaa usipofanya hivyo utajikuta umetumbukia kwenye shimo bila kutarajia.
Kwingineko unaweza kukanyaga kinyesi au kitu kinachoweza kukudhuru. Aidha baiskeli, mikokoteni na magari yako huru kupita hata unakojificha.
VIJIJINI
UMASIKINI kwa wakazi wa maeneo pembeni ya bahari ni wa kujitakia ? Pengine. Kuna hoteli ya Mzungu huko Saadani imejengwa kwa makuti, majamvi na mkeka. Kila kinachotumika hotelini kinatengenezwa au kulimwa au kuvuliwa na wanakijiji wenyewe. Amkeni mlio kando ya bahari mnaweza kuwa wamiliki wa hoteli za kitalii eti!
Barua-pepe: ishi.jamboleo@gmail.com
WATU wengi hudhani kulipiza kisasi au kumtendea ubaya aliyekutendea ubaya ndio jambo linalofaa. Jaribu kutolipiza kisasi na umtendee wema aliyekutendea ubaya. Lazima lipo litakalokushangaza tu.
NYUMBANI
ISRAFU ni matumizi mabaya kwa kile mnachoruzukiwa na aliyewaumba. Wafundishe jamaa yako 'uchumi' katika matumizi. Ziada inayozidi inaweza ikatolewa kwa wahitaji kwa baraka zaidi kwa familia yenu. Israfu ikiendelea bila kudhibitiwa hujenga familia isiyojali na isiyo na huruma.
NJIANI
KUWA mwangalifu na waendesha baiskeli na vijana wenye magurudumu miguuni. Tahadhari inahitajika sio tu kujihami mwenyewe bali pia kukuepusha wewe kuwa chanzo cha umauti au ulemavu kwa hao wapanda baiskeli na waburuza 'rolasketi' .
SAFARINI
SAFARINI huweza kugeuzwa sadaka au ibada ya aina fulani. Ukisafiri jenga mazoea ya kuulizia ndugu, jamaa au Watanzania wenzako wanapoishi. Kwalo hilo unaweza kupeleka faraja kwa wenye dhiki au maradhi. Na kama sehemu unaijua ni vizuri pia kutembelea hospitali za karibu. Afya yako ya mwili na akili yaweza kuimarika kwa hili.
KAZINI
MAHALA pa kazi huweza kugeuzwa kituo kizuri cha upatu au SACCOS jinsi mnavyotaka wenyewe. Ili mradi tu kuchagua watu waaminifu kusimamia shughuli yenyewe. Kuchanga shilingi elfu moja au mbili kwa wiki kunaweza kuja kukusaidia katika shida usiyotegemea.
SHULENI
KUSOMA sana sio kufaulu sana. Watazame wanaobukua usiku na mchana ulinganishe na matokeo yao bila shaka utawasikitikia. Kusoma kunahitaji kuweka mikakati na kutumia akili zaidi ya darasani.
NCHI ZA NJE
KAZI nyingine za nje ni kuwa boi au yaya nyumbani kwa mtu. Tofauti na hapa Tanzania ni ule ukweli kuwa mshahara ni mzuri na unaweza ukatuma fedha nyumbani. Ili mradi upate mwajiri anayemwogopa Mungu. Vinginevyo unaweza kunyanyasika huko kiasi cha kutisha. Chunguza kwanza kabla ya kuamua.
BURUDANI
Mchezo wa kurusha vishale (darts) ni burudani kwa watu wanaopenda starehe ya mchezo wa kikundi. Katika burudani hii unaweza kuzungumza na marafiki na jamaa; unaweza kunywa na mnaweza mkapanga mambo mbali mbali ya kufanya siku zijazo. Ni burudani inayochochea uvumbuzi, uzuzi na ujasiriamali.
MICHEZONI
WANAOHARIBU michezo wakati mwingine ni waandishi wa habari na vyombo vyao. Hivi sasa baadhi yao wanafundisha kuliko kocha, wanacheza kuliko mchezaji bora; na ni waamuzi wa kutegemea kuliko waamuzi wa mechi husika. Hili halisaidii michezo. Linabomoa michezo.
MJINI
KATIKA miji yetu mingi hivi sasa jenga mazoea ya kutazama mguu wako unakotua. Katika baadhi ya mitaa usipofanya hivyo utajikuta umetumbukia kwenye shimo bila kutarajia.
Kwingineko unaweza kukanyaga kinyesi au kitu kinachoweza kukudhuru. Aidha baiskeli, mikokoteni na magari yako huru kupita hata unakojificha.
VIJIJINI
UMASIKINI kwa wakazi wa maeneo pembeni ya bahari ni wa kujitakia ? Pengine. Kuna hoteli ya Mzungu huko Saadani imejengwa kwa makuti, majamvi na mkeka. Kila kinachotumika hotelini kinatengenezwa au kulimwa au kuvuliwa na wanakijiji wenyewe. Amkeni mlio kando ya bahari mnaweza kuwa wamiliki wa hoteli za kitalii eti!
Barua-pepe: ishi.jamboleo@gmail.com
ishi - Desemba 1, 2009
BINAFSI
NAFSI inasemekana iko katika daraja tatu. Daraja la chini kabisa ni la nafsi
inayojifikiria yenyewe daima na kutaka kujitosheleza mara moja kwa lolote lile.
Nafsi ya pili ni ile inayojua sio rahisi kujitosheleza mara moja nyakati zote. Na
ile ya juu kabisa ni ile inayojua kusimamia nafsi ya kwanza na ya pili ili
mustakabali wa mtu binafsi sikuzote uwe bora.
*******************************************************************************
NYUMBANI
NYUMBA mnayoishi ndiyo Ikulu ya wanafamilia. Heshima yake lazima iwe juu ya heshima kwa sehemu nyingine yoyote. Hapa ndio kimbilio la wote kwa yote wanayokutana nayo katika shughuli zao za maisha ya kila siku. Amani na utulivu ni muhimu kutawala mahala hapa. Isipokuwa hivyo sio rahisi kwa anayetoka nyumba hiyo kufanikiwa katika lolote lile.
*********************************************************************************
NJIANI
NJIA ni mapito ya kila mtu. Haifai kwa yeyote yule kudhani au kutenda jambo
linaloonesha kana kwamba njia ni yake na mwenzie tu. Onyesha utu na tumia busara unapokuwa njiani kuwaachia watu wengine nao nafasi ya kuitumia kama wewe usivyopendwa kukwazwa na mtumia njia mwingine.
*********************************************************************************
SAFARINI
UNAPOKUWA safarini ni vizuri kufahamiana na msafiri au wasafiri wenzako. Tendo hili huwa gumu kwa wengine hadi pale wanapopatwa na shida fulani. Usingoje shida kukufikandiyo umjue msafiri mwenzio. Busara na hekima zinaonesha wanaowasalimia wasafiri wenzao hata wale wasiowajua huwa na safari njema na bora zaidi.
********************************************************************************
SHULENI
Shuleni ni mahala pa kuafuta elimu. Sio mahala pa kujionesha au pa kushughulika na yale yasiyochangia lolote kuoneza elimu au maarifa yako. Upo ushahidi wa kutosha kwamba wale wanaofika shuleni kwa malengo mengine badala ya yale yaliyokusudiwa, yaani, kuelimika, huwa na wakati mgumu shuleni.
********************************************************************************
KAZINI
KAZI yoyote ile ni mkataba wa hiari kati ya mtoa ajira na mwajiriwa. Kabla hujafanya maamuzi ya kuwa mwajiriwa wa sehemu fulani hakikisha kwamba maslahi na matarajio yako yatafikiwa kwa kukubali kuajiriwa na mwajiriwa fulani. Vinginevyo huko mbele ya safari utakapoona maslahi yako ni duni na matarajio yako mengi ni njozi utajidhalilisha mwenyewe na yule aliyekuajiri.
*******************************************************************************
NCHI ZA NJE
UKIWA nchi za nje ni vizuri utumie siku zako za kwanza kuwajua wenyeji wako na mazingira yako. Hata kabla hujaondoka kwenu ni vizuri upate habari za kule
unakokwenda. Hili litakusaidia kupata mwanga wa tabia na mienendo ya wenyeji wako. Vinginevyo unaweza kujikuta mengi yanakuharibikia kwa kuwa tu hujawajua wenyeji wako na mazingira yako ipasavyo.
********************************************************************************
BURUDANI
BURUDANI ya kweli sio lazima iwe inayotumia fedha. Burudani ni jambo lolote lile linalokutoa katika mazingira ya mihemuko na shiniko za kazi au shughuli za kawaida na kukupeleka mahala kwenye utulivu au msisimko fulani unaokukurubisha wewe na mazingira yako au yule au wale uwapendao na hivyo kupata fursa ya kuibwaga chini mizigo ya maisha unayoibeba kila siku katika siku zako za kazi, masomo au shughuli nyingine yoyote ile iwayo.
********************************************************************************
MICHEZONI
MICHEZO huanza kwa kuwa na sehemu ya michezo. Jamii inayoshindwa kuwa na sehemu ya michezo ni jamii ya kishenzi na iliyo nyuma sana kimaendeleo. Wahenga walituambia kuwa malezi ya watoto na vijana bila shughuli za kuwapotezea muda ni kitu kigumu na chenye hatari ya kuingiliwa na shetani wakati wowote ule. Tuajribu kuhimiza kuwepo kwa viwanja vya michezo kwa kila kata kama sio mtaa kote nchini.
********************************************************************************
MJINI
MJINI ni sehemu ambayo imani, amani, wema, ukarimu na ucha Mungu huwa mdogo sana kwa sababu ya ushindani, wivu, kuiga, tamaa na watu kutaka kujionesha.
Maisha bora hayapatikani kwa kuiga wengine na kutaka kuwa wao. Maisha bora
hupatikana kwa wewe kuwa kile unachostahili kuwa na sio vinginevyo. Muigaji siku zote ni nyani. Mwenye lake la asili hata kama sio bora wala zuri sana ana heshima mara kadhaa kuliko mwigizaji wa kile anachodhani ni bora na zuri zaidi. Turingie kilicho chetu, turingie asili yetu.
********************************************************************************
VIJIJINI
MAISHA ya mjini ni ya mwendo mdebwedo na ndivyo yanavyostahili kuwa. Ni heri kwako kwenda nao kuliko wewe kutaka waige mwendo wako wa mjini na wa kimaendeleo.
Katika hili kuna sili ya asili na fasili. Polepole ya mwanakijiji ndio mwendo wa
asili wa binadamu. Haraka haraka ya mjini ni kielelezo ya jitihada kama zile za mbio za farasi sakafuni.
********************************************************************************
NAFSI inasemekana iko katika daraja tatu. Daraja la chini kabisa ni la nafsi
inayojifikiria yenyewe daima na kutaka kujitosheleza mara moja kwa lolote lile.
Nafsi ya pili ni ile inayojua sio rahisi kujitosheleza mara moja nyakati zote. Na
ile ya juu kabisa ni ile inayojua kusimamia nafsi ya kwanza na ya pili ili
mustakabali wa mtu binafsi sikuzote uwe bora.
*******************************************************************************
NYUMBANI
NYUMBA mnayoishi ndiyo Ikulu ya wanafamilia. Heshima yake lazima iwe juu ya heshima kwa sehemu nyingine yoyote. Hapa ndio kimbilio la wote kwa yote wanayokutana nayo katika shughuli zao za maisha ya kila siku. Amani na utulivu ni muhimu kutawala mahala hapa. Isipokuwa hivyo sio rahisi kwa anayetoka nyumba hiyo kufanikiwa katika lolote lile.
*********************************************************************************
NJIANI
NJIA ni mapito ya kila mtu. Haifai kwa yeyote yule kudhani au kutenda jambo
linaloonesha kana kwamba njia ni yake na mwenzie tu. Onyesha utu na tumia busara unapokuwa njiani kuwaachia watu wengine nao nafasi ya kuitumia kama wewe usivyopendwa kukwazwa na mtumia njia mwingine.
*********************************************************************************
SAFARINI
UNAPOKUWA safarini ni vizuri kufahamiana na msafiri au wasafiri wenzako. Tendo hili huwa gumu kwa wengine hadi pale wanapopatwa na shida fulani. Usingoje shida kukufikandiyo umjue msafiri mwenzio. Busara na hekima zinaonesha wanaowasalimia wasafiri wenzao hata wale wasiowajua huwa na safari njema na bora zaidi.
********************************************************************************
SHULENI
Shuleni ni mahala pa kuafuta elimu. Sio mahala pa kujionesha au pa kushughulika na yale yasiyochangia lolote kuoneza elimu au maarifa yako. Upo ushahidi wa kutosha kwamba wale wanaofika shuleni kwa malengo mengine badala ya yale yaliyokusudiwa, yaani, kuelimika, huwa na wakati mgumu shuleni.
********************************************************************************
KAZINI
KAZI yoyote ile ni mkataba wa hiari kati ya mtoa ajira na mwajiriwa. Kabla hujafanya maamuzi ya kuwa mwajiriwa wa sehemu fulani hakikisha kwamba maslahi na matarajio yako yatafikiwa kwa kukubali kuajiriwa na mwajiriwa fulani. Vinginevyo huko mbele ya safari utakapoona maslahi yako ni duni na matarajio yako mengi ni njozi utajidhalilisha mwenyewe na yule aliyekuajiri.
*******************************************************************************
NCHI ZA NJE
UKIWA nchi za nje ni vizuri utumie siku zako za kwanza kuwajua wenyeji wako na mazingira yako. Hata kabla hujaondoka kwenu ni vizuri upate habari za kule
unakokwenda. Hili litakusaidia kupata mwanga wa tabia na mienendo ya wenyeji wako. Vinginevyo unaweza kujikuta mengi yanakuharibikia kwa kuwa tu hujawajua wenyeji wako na mazingira yako ipasavyo.
********************************************************************************
BURUDANI
BURUDANI ya kweli sio lazima iwe inayotumia fedha. Burudani ni jambo lolote lile linalokutoa katika mazingira ya mihemuko na shiniko za kazi au shughuli za kawaida na kukupeleka mahala kwenye utulivu au msisimko fulani unaokukurubisha wewe na mazingira yako au yule au wale uwapendao na hivyo kupata fursa ya kuibwaga chini mizigo ya maisha unayoibeba kila siku katika siku zako za kazi, masomo au shughuli nyingine yoyote ile iwayo.
********************************************************************************
MICHEZONI
MICHEZO huanza kwa kuwa na sehemu ya michezo. Jamii inayoshindwa kuwa na sehemu ya michezo ni jamii ya kishenzi na iliyo nyuma sana kimaendeleo. Wahenga walituambia kuwa malezi ya watoto na vijana bila shughuli za kuwapotezea muda ni kitu kigumu na chenye hatari ya kuingiliwa na shetani wakati wowote ule. Tuajribu kuhimiza kuwepo kwa viwanja vya michezo kwa kila kata kama sio mtaa kote nchini.
********************************************************************************
MJINI
MJINI ni sehemu ambayo imani, amani, wema, ukarimu na ucha Mungu huwa mdogo sana kwa sababu ya ushindani, wivu, kuiga, tamaa na watu kutaka kujionesha.
Maisha bora hayapatikani kwa kuiga wengine na kutaka kuwa wao. Maisha bora
hupatikana kwa wewe kuwa kile unachostahili kuwa na sio vinginevyo. Muigaji siku zote ni nyani. Mwenye lake la asili hata kama sio bora wala zuri sana ana heshima mara kadhaa kuliko mwigizaji wa kile anachodhani ni bora na zuri zaidi. Turingie kilicho chetu, turingie asili yetu.
********************************************************************************
VIJIJINI
MAISHA ya mjini ni ya mwendo mdebwedo na ndivyo yanavyostahili kuwa. Ni heri kwako kwenda nao kuliko wewe kutaka waige mwendo wako wa mjini na wa kimaendeleo.
Katika hili kuna sili ya asili na fasili. Polepole ya mwanakijiji ndio mwendo wa
asili wa binadamu. Haraka haraka ya mjini ni kielelezo ya jitihada kama zile za mbio za farasi sakafuni.
********************************************************************************
Subscribe to:
Posts (Atom)
